π¨_|| ππππ₯ π ππ π ♥️π₯Ί
➡️ Mwambie anipigie ni mimi mama yake!!
➡️ Mwambie sina simu ila nimeona picha zake kwenye simu ya kupalaza ya khamisi.Mwambie amenenepa sana
➡️ Mwambie nimeona gari lake ni zuri sana !!ila mwambie mama yake bado naishi kwenye lile banda pamoja na kuku.
➡️ Mwambie nimeumwa sana ila nikapona bila hata kutumia dawa.
➡️ Mwambie mzee juma bado ananidai pesa zake nilizokopa ili nimlipie ada amechukua kile kishamba nilichokuwa nakitegemea kufidia deni lake.
➡️ Mwambie mimi mama yake nimebaki pekee yangu tangu baba yake kafariki sina hata wa kunisogezea kuni motoni.
➡️ Mwambie leo nimetamani sana nyamaπ zile mboga zilizoota zenyewe upenuni zimenichosha mpka mdomo umekuwa mchungu.
➡️ Mwambie wale vijana walitaka wanipige eti mimi mchawi.
➡️ Mwambie mama yake nimekuwa mzee sana nahesabu siku tu aje hata nishike mikono yake nimuoneshe mipaka ya nyumba yetu/!!
➡️ Salio limeisha mwambie mama anampenda sanaπ!ila huku kijijini nimebaki pekee yangu wenzangu wote wameenda mjini kusherekea kwa watoto wao...
π’π’ TUSIWASAHAU WAZAZI WAKUU ππππΎ

No comments:
Post a Comment